MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII
TANGAZA NASI MATANGAZO YA KIJAMII BURE KUPITIA BLOG HII

Alhamisi, 2 Aprili 2015

SHIGONGO AZINDUA SEMINA YA UJASILIAMALI TANDALE-DAR


                    Wahamasishaji maarufu wa ujasiliamali Afrika Mashariki na Kati, Eric Shigongo    na James James Mwang’amba wakiwasalimia umati kabla ya kuanza semina.

LET SHARE ................................

Wahamasishaji maarufu wa ujasiliamali Afrika Mashariki na Kati, Eric Shigongo na James James Mwang’amba wakiwasalimia umati kabla ya kuanza semina.
Shigongo akioa somo kwenye semina hiyo.
.....Akiendelea kuwafundisha mbinu za kujikwamua kwenye umaskini na kuwa tajili.
Umati ukiwa umefurika.
Mkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers, Eric Shigongo (kulia) na Mkurugenzi wa Mwang’amba Communication LTD, James Mwang’amba (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na kijana mwenye ndoto za kuwa mjasilamali kabla ya kuanza semina.
Shigongo akipeana mkono na mmoja kati ya vijana wa Tandale waliofika kiwanjani hapo kufuatilia semina ya ujasiliamari.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Pamela Dafa 'Pam D' akitoa burudani wakati wa semina hiyo.
Pam D akiendelea kutoa burudani.
Wasanii Chipukizi wa Tandale wakitoa burudani katika semina hiyo.

MKURUGENZI  Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers, Eric Shigongo amezindua Semina ya Ujasiliamali katika Uwanja wa Shule ya Msingi Tandale jijini Dar es Salaam jana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu.

Uzinduzi huo ulifanyika kuanzia  saa nane na nusu mchana katika huo ambapo Shigongo akiambatana na wajasiliamali, James Mwang’amba  ambaye ni Mkurugenzi wa Mwang’amba Communication LTD pamoja na Dk. Didas Lunyungu, Mkurugenzi Mjasiriamali Kwanza Enterprises LTD ambao nao wanatoa elimu katika semina hiyo.

Katika uzinduzi huo  Shigongo ndiye aliyeanza kuzungumza ,alianza kwa kuelezea historia ya maisha yake kwa ufupi huku akifafanua kuwa ni dhahiri kila mmoja sasa ni wakati wake kufanya mabadiliko katika kubadili maisha yake.

Alisema kuwa yeye ni mmoja wa watu waliotoka katika maisha ya umaskini, manyanyaso na hata kuitwa majina ya kuashiria hali ya maisha ya ufukara kwa kuitwa majina kama, Madaso akimaanisha mtu anayevaa nguo zilizochanika na akaamua mkoani Mwanza na kwenda jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutafuta maisha huku akilala katika stendi ya daradala ya Kisutu Posta.

Alifafanua kuwa aliweza kutoka katika hali aliyokuwa nayo na sasa kuwa katika hali ya unafuu, hivyo  sasa Tandale atatoa mafunzo katika semina hiyo ambayo yataweza kuwasaidia wakazi wa eneo hilo kutoka katika maisha waliyonayo na kuwa katika sehemu nyingine.

Alielezea namna maeneo hayo ya Tandale yanavyosahaulika hata katika mgao wa umeme ukilinganisha na Masaki e ,Masaki na hata maeneo mengine,hivyo sasa alisema sasa ni wakati mufaka kwa wananchi hao kujifunza siri ya utajiri.
Aliwaeleza jinsi alivyoanza kuandika vitabu vyake na kuviuza bila kusoma vya wengine kama njia mojawapo ya ujasiliamali.

Nao James Mwang’amba pamoja na Dk.Didas Lunyungu wote kwa pamoja waliweza kusalimiana na waliohudhuria semina hiyo na kutoa ufafanuzi kwa ufupi huku, wakielezea namna walivyojipanga katika kutoa mafunzo leo  ambayo yatawatoa katika sehemu waliyopo na kuwa katika sehemu nyingine ya kimaendeleo.

Semina hiyo itaendelea leo katika uwanja huo kuanzia saa 8:30 mchana mpaka 12 jioni,na pia itakuwepo kesho mpaka siku ya mwisho ambayo itakuwa ni Jumamosi Aprili 4.
PICHA/STORI NA DENIS MTIMA/GPL

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni