MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII
TANGAZA NASI MATANGAZO YA KIJAMII BURE KUPITIA BLOG HII

Jumapili, 12 Aprili 2015

Obama na Castro wafanya mkutano.

                      Rais Obama na Castro wakiamukuana

Viongozi wa marekani na Cuba wamefanya mkutano wao wa kwanza tangu zaidi ya nusu karne iliyopita.

Rais Obama na mwenzake wa Cuba Raul Castro walikutana ana kwa ana pembezoni mwa mkutano wa nchi za Amerika nchini Panama.

Mkutano huo utatoa mwelekeo wa kuboresha uhusiano baada ya miongo kadha ya uhasama kati ya Marekani na kisiwa hicho cha utawala wa kikoministi

Rais Obama alisema kuwa angependa kuona watu wa Cuba wakiendelea kuishi kwa uhuru na kwa usalama. Naye Castro kwa upande wake alisema kuwa Cuba ilikuwa tarayi kujenga urafiki na marekni lakini akaongeza kuwa nchi hizo mbili zina tofauti nyingi na historia iliyokumbwa na utata.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni