MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII
TANGAZA NASI MATANGAZO YA KIJAMII BURE KUPITIA BLOG HII

Jumapili, 12 Aprili 2015

Wakimbizi wa Somalia:Kenya yaonya UN


 Wakimbizi wa Somalia katika kambi ya wakimbizi wa Daadab nchini Kenya

Serikali ya Kenya imeupatia Umoja wa Mataifa makataa ya miezi mitatu kuwahamisha wakimbizi wa Somalia wapatao nusu milioni hadi nchini Somalia.
Naibu rais William Ruto amesema kuwa iwapo Umoja wa mataifa utakataa kuwahamisha wakimbizi hao, Kenya itachukua jukumu la kuwandoa.
Makataa hayo yanajiri siku kadhaa baada ya shambulizi la chuo kikuu cha Garissa ambapo takriban watu 148 waliuawa na kundi la wapiganaji wa Al-shaabab.
                                 Wakimbizi Dadaab
Baadhi ya wakimbizi wamekuwa wakiishi katika kambi za Dadaab mashariki ya taifa hilo kwa zaidi ya miongo miwili.
Kenya imelishtumu kundi la Alshabaab kwa kujificha katika kambi hizo huku likiwasajili wanachama wapya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni