MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII
TANGAZA NASI MATANGAZO YA KIJAMII BURE KUPITIA BLOG HII

Jumanne, 14 Aprili 2015

WB: Tanzania bado ngangari kiuchumi.

                  Waziri wa fedha Tanzania Saada Mkuya.

Utafiti uliofanywa na Benki Kuu ya Dunia kwa robo ya kwanza ya mwaka kuhusu hali ya kiuchumi barani Afrika, umeonyesha kuwa Tanzania ni kati ya nchi barani humo  ambazo bado zipo imara kiuchumi ndani ya kipindi hicho.
 
Hata hivyo, baadhi ya nchi zikiwamo zinazozalisha na kusafirisha kwa wingi nje bidhaa ya mafuta, zinatarajia kuonja makali ya mdodoro wa uchumi ndani ya mataifa hayo tangu kipindi hiki hadi mwaka ujao.
 
Matokeo ya utafiti huo kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015, yaliyotolewa jana na taasisi hiyo ya fedha duniani kwa kurushwa moja kwa moja kwa nchi zote zilizopo kusini mwa Jangwa la Sahara, Tanzania ikiwamo , kutoka Washington DC, Marekani.
 
Akitoa taarifa hiyo, Mchumi kiongozi wa Benki ya Dunia (WB), kwa upande wa Bara la Afrika, Punan Chuhan, alitaja nchi ambazo zinajimudu kiuchumi mpaka sasa kuwa ni Ivory Coast, Tanzania na Msumbiji.
 
Alitaja baadhi ya sababu kwa nchi hizo hasa Tanzania kubaki katika hali nzuri wakati nyingine zikiteseka, kuwa ni miundombinu imara na utengemavu katika shuguli za uchimbaji wa madini.
 
Hata hivyo, huo wa kwanza kutolewa na benki hiyo ya dunia  barani humo kwa mwaka huu kulingana na utaratibu wake, inaonyesha kuwa hali ya uchumi kwa ujumla barani humo imeshuka kutoka asilimia 4.5 mwaka uliopita hadi asilimia 4 mwaka huu.
      Na Isaya Kisimbilu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni