Rais Jakaya Kikwete jana amepokea Ripoti ya Uchunguzi wa Operesheni Tokomeza, katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam.
Akipokea ripoti hiyo, Rais Kikwete ameishukuru Tume kwa kazi nzuri
na kuongeza kuwa amefurahi kuwa suala zima la Operesheni Tokomeza
limefikia mwisho wake.
Aidha, Rais alisema kuwa serikali itaisoma ripoti hiyo na katika
kipindi cha wiki mbili itatoa maelezo ya jinsi itakavyoshughulikiwa.
Alipokea ripoti hiyo kutoka kwa Balozi Jaji (mstaafu) Hamisi Msumi,
Mwenyekiti wa Tume ambayo Rais Kikwete aliiteua Mei mosi, mwaka jana,
na kuitaka ichunguze tuhuma mbalimbali za uvunjifu wa sheria, kanuni,
taratibu na hadidu za rejea za utekelezaji wa Operesheni Tokomeza.
Aidha, aliipa Tume hiyo jukumu la kupendekeza hatua stahiki za
kisheria za kuchukua dhidi ya watakaobainika kuhusika na uvunjifu huo.
Vile vile, Rais aliiagiza Tume hiyo ishauri namna bora ya utekelezaji wa
Operesheni kama hiyo hapo baadaye.
Rais Kikwete pia aliipa Tume hiyo Hadidu za Rejea sita ambazo pia ziliainishwa katika Taarifa ya Serikali Namba 131 ya 2014.
Hadidu hizo ni kuchunguza namna Operesheni Tokomeza
ilivyotekelezwa; Ambazo ni kuchunguza iwapo maafisa waliotekeleza
Operesheni Tomokeza walizingatia sheria, kanuni, taratibu na hadidu za
rejea walizopewa;
kama maofisa waliotekeleza Operesheni Tokomeza, kuna watu
waliokiuka sheria yoyote wakati wa kupendekeza hatua zinazostahili
kuchukuliwa dhidi ya maafisa wa (f) Kupendekeza mambo yanayopaswa
kuzingatiwa wakati wa kupanga na kama walivunja sheria, kanuni, taratibu
na hadidu rejea walizopewa.
Utekelezaji wa Operesheni Tokomeza na hatua zilizochukuliwa na
maofisa wa Operesheni Tokomeza dhidi ya wakosaji hao na mali zao
zilikuwa sahihi; Operesheni Tokomeza waliokiuka sheria, kanuni, taratibu
na hadidu za rejea za Operesheni hiyo; na kutekeleza Operesheni
nyingine kama hii, ili kuepuka malalamiko mengine yasitokee.
Jaji Msumi alimweleza Rais Kikwete kuwa Tume ilitembelea mikoa 20
na wilaya 38 na kupokea malalamiko mbali mbali kutoka kwa Viongozi wa
Serikali wakiwamo mawaziri wanne waliojiuzulu, watekelezaji wa
Operesheni; na walalamikaji/wahanga wa Operesheni.
Jaji Msumi alimweleza Rais Kikwete kuwa Ripoti ya Tume ina Juzuu
kumi, ikiwamo muhtasari wa Taarifa ya Tume, Taarifa yenyewe ya Tume na
Juzuu ya tatu hadi ya tisa ikiwa ni Mwenendo wa Ushahidi (Proceedings)
ambapo Juzuu ya kumi ikiwa ni vielelezo vilivyotolewa na mashahidi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni