MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII
TANGAZA NASI MATANGAZO YA KIJAMII BURE KUPITIA BLOG HII

Jumapili, 19 Aprili 2015

Obama: mabadiliko ya hewa hayakanushiki



Rais Obama ameonya kuwa mabadiliko ya hali ya hewa hayawezi tena kukanushwa au kudharauliwa, na amesema ndio tishio kubwa kabisa linalokabili dunia.
Katika hotuba yake ya kila juma, Rais Obama alisema anataka aweze kuwatazama watoto na wajuukuu wake machoni na kusema kuwa kila liwezalo limefanywa kupambana na msukosuko huo.
Bwana Obama hivi karibuni aliahidi kupunguza sana kiwango cha gesi inayozidisha joto inayotolewa na Marekani - kiwango cha pili kikubwa kabisa duniani - kabla ya mkutano wa viongozi wa dunia mwezi wa Disemba.
Mipango yake inapingwa vikali na wanasiasa wengi wa chama cha Republican ambao wanadai kuwa itaumiza makampuni ya Marekani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni