MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII
TANGAZA NASI MATANGAZO YA KIJAMII BURE KUPITIA BLOG HII

Jumapili, 17 Mei 2015

MLIPUKO WA BOMU WAUA WATATU KABUL

Mmoja wa majeruhi katika shambulio hilo akitolewa eneo la tukio.
Baadhi ya magari yaliyoteketea kutokana na shambulio hilo.
Mama huyu akitolewa eneo la mlipuko na kupelekwa sehemu salama.
WATU watatu wameripotiwa kupoteza maisha huku wengine takribani 20 wakijeruhiwa baada ya mlipuko kutokea kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa mjini Kabul nchini Afghanistan leo.
Mashuhuda wa tukio hilo wanasema kuwa mlipuaji wa bomu hilo la kujitolea muhanga alikuwa amelenga wanajeshi wa kimataifa nje ya lango kuu la uwanja huo wa ndege.
Lango hilo hutumika na vikosi vya kijeshi vya kigeni. Kundi la Taliban limethibitisha kuhusika na shambulio hilo katika taarifa yake lililoituma kwa wanahabari.
Shambulizi hilo linafanyika ikiwa ni siku tatu baada ya mwanamgambo mmoja wa Taliban kuwaua watu 14 wakiwemo raia tisa wa kigeni katika hoteli moja mjini humo.

Chanzo: BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni