MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII
TANGAZA NASI MATANGAZO YA KIJAMII BURE KUPITIA BLOG HII

Jumanne, 19 Mei 2015

Mji wa Ramadi watorokwa Iraq

                                                   MJi wa Ramadi wasalia bila watu

Maelfu ya raia wa Iraq wanaendelea kuukimbia mji wa Ramadi huku kundi la wanamgambo wa Islamic State likiwazuia na kuendeleza mashambulizi ya kuudhibiti mji wa Ramadi.

Waasi hao wameuteka mji huo kutoka kwa vikosi vya serikali.
Umoja wa mataifa unasema kuwa watu elfu 25 wameutoroka mji huo katika siku kadhaa zilizopita, wakielekea mashariki hadi mjini Baghdad.

Raia wapatao elfu mia moja na thelathini walitoroka mji huo mwezi uliopita, ulipovamiwa na kundi la Islamic State.

Shirika la umoja wa mataifa pamoja na mashirika mengine, yameanza kusambaza chakula, maji na dawa, huku pia kambi za muda zikijengwa.
NA BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni