MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII
TANGAZA NASI MATANGAZO YA KIJAMII BURE KUPITIA BLOG HII

Jumapili, 29 Machi 2015

Rais Mugabe ahimiza uhusiano wa China, Afrika.




Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, amewataka vijana  kudumisha ushirikiano uliopo kati ya Afrika  na China kwani ndiyo nchi pekee duniani ambayo imeonyesha kuwa ni rafiki wa kweli wa  Bara la Afrika.
 
Rais Mugabe alitoa wito huo jijini Arusha jana, alipokuwa akifungua Kongamano la Viongozi wa Vijana  wa Afrika  na China.
 
Kongamano hilo linashirikisha  washiriki  4,000 kutoka mataifa 40 ya Afrika likiwa na lengo la kujadili changamoto zinazowakabili Vijana kwenye ulimwengu wa kibepari na namna bora  ya kuvutia  wawekezaji kuja kuwekeza Afrika.
 
Alisema mahusiano kati ya Afrika na China yalianza muda mrefu na yataendelea kwa vizazi vijavyo.
 
Rais Mugabe alisisitiza kwamba China ni rafiki wa kweli wa Afrika na urafiki huu utaendelea kudumishwa na kuuendelezwa kwa faida ya vizazi vijavyo.
Mugabe  aliisifia Serikali ya China kwa kusaidia Bara la Afrika tangu harakati za ukombozi hadi sasa.
 
Mugabe amewaambia vijana hao kuwa  China bado inaendeleza harakati zake za kusaidia Bara la Afrika katika utekelezaji wa programu mbalimbali za maendeleo, kiuchumi na kijamii mchango ambao watu wa Afrika na hususan Vijana wanapaswa kuuthamini.
 
Alisema China iliisaidia Tanzania  na Zambia  wakati wa ujenzi wa reli ya Uhuru (Tazara), ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Dar es Salaam kwenda Kapiri Mposhi, Zambia (Tazama).
 
Pia China ilisaidia ujenzi wa mradi wa kiwanda cha urafiki pamoja na mradi wa makaa ya mawe  wa Kiwira mkoani Mbeya pamoja na uanzishaji wa mradi wa kilimo cha mpunga Mbarali.
 
Alisema nchi hiyo imesaidia miradi mingi  barani Afrika
Aliwataka Vijana wa Afrika na China kuimarisha ushirikiano kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Kikomunist cha Watu wa China (CPC).
 
Alisema Afrika bado inakabiliwa na changamoto nyingi hususan  suala la ukosefu wa  ajira kwa vijana hivyo kongamano hilo litafute njia za kupata ufumbuzi  wa namna  ya kuwawezesha vijana kupata ajira kwa kuanzisha miradi ya kiuchumi itakayowawezesha vijana wa Afrika kujiajiri.
    Na Cynthia Mwilolezi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni