MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII
TANGAZA NASI MATANGAZO YA KIJAMII BURE KUPITIA BLOG HII

Alhamisi, 16 Julai 2015

Viongozi 2 wa Alshabaab wauawa kwa bomu



Viongozi wawili wa kundi la wapiganaji wa kiislamu wa Al shabaab nchini Somalia wameuawa kwenye shambulio la mabomu ya angani.
Watu katika mji wa Baardhere ulioko kusini mwa nchi hiyo wanasema walisikia milipuko asubuhi ya leo katika eneo hilo.
Kisha wapiganaji hao wa Al shabaab wakafika eneo hilo la tukio.
Baardheere ni moja ya miji ambayo bado ingali inadhibitiwa na wapiganaji wa Al shabaab.
Wanajeshi wa muungano wa Afrika na wale wa serikali ya Somalia wanakaribia eneo hilo.
Viongozi kadhaa wa kundi hilo wameuawa kwenye mashambulio ya mabomu ya angani yaliyoangushwa na wanajeshi wa Marekani.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni