MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII
TANGAZA NASI MATANGAZO YA KIJAMII BURE KUPITIA BLOG HII

Alhamisi, 16 Julai 2015

Jeshi la Japan sasa kupigana nje



Bunge la uwakilishi la Japan, limeidhinisha kifungu cha sheria ya usalama yenye utata inayoleta mabadiliko inayoliruhusu jeshi la nchi hiyo kupigana katika mataifa ya kigeni tangu wakati wa kumalizika kwa vita vya pili vya dunia.
Mabadiliko hayo ambayo yalipigiwa upatu na waziri mkuu Shinzo Abe, ambaye anasema kuwa itairuhusu Japan kukabiliana na vitisho hasa kutoka China.
null
Jeshi la Japan
Msemaji wa wizara ya mashauri ya nchi za kigeni Hua Chunying, ameitaka Japan isalie katika njia ya maendeleo ya amani na kusaidia majirani zake.
Mabadiliko hayo yalianzishwa na waziri mkuu, Shinzo Abe, anayeamini kuwa ni muhimu kukabiliana na changamoto mpya inayoikabili Japan, hasa kutoka China.
Lakini wapinzani wanaamini kuwa marekebisho hayo, yanakiuka katiba ya Japan iliyobuniwa baada ya vita na inaweza kuyumbisha usalama wa taifa hilo, katika mzozo unaoongozwa na Marekani.
null
Raia wa Japan wapinga sheria ya kuliruhusu taifa hilo kushiriki katika vita vya kimataifa
Baada ya hotuba kadhaa wakati wa mjadala huo bungeni, vyama vya upinzani vilikataa kuhudhuria shughuli za upigaji kura.
Kumeshuhudiwa upinzani mkali dhidi ya mabadiliko hayo, hali iliyosababisha kushuka kwa umaarufu wa bwana Abe.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni